TOPIC 3: UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI SIMULIZI
Fasihi
simulizi kama zilivyo kazi nyingine za fasihi andishi hufanyiwa uhakiki.
Uhakiki huu huzingatia vipengele vya fani na maudhui ili kubainisha usanaa wa
kazi husika pamoja na kile ilichokusudia kufikishwa kwa hadhira.
simulizi kama zilivyo kazi nyingine za fasihi andishi hufanyiwa uhakiki.
Uhakiki huu huzingatia vipengele vya fani na maudhui ili kubainisha usanaa wa
kazi husika pamoja na kile ilichokusudia kufikishwa kwa hadhira.
UHAKIKI WA USHAIRI
Mashairi
kama kazi nyingine za kifasihi huhakikiwa kwa kutumia vigezo sawa na
vinavyotumika katika kazi nyingine za kifasihi. Vigezo hivyo ni kwa kuzingatia
vipengele vyake viwili yaani fani na maudhui.
kama kazi nyingine za kifasihi huhakikiwa kwa kutumia vigezo sawa na
vinavyotumika katika kazi nyingine za kifasihi. Vigezo hivyo ni kwa kuzingatia
vipengele vyake viwili yaani fani na maudhui.
VIPENGELE VYA FANI
Uhakiki
wa fani za ushairi ni uchambuzi wa kina na kuziweka wazi mbinu za kisanaa
alizotumia mshairi katika kutunga kazi yake. Vipengele muhimu vya kuhakiki
katika fani ya ushairi ni kama vifuatavyo:
wa fani za ushairi ni uchambuzi wa kina na kuziweka wazi mbinu za kisanaa
alizotumia mshairi katika kutunga kazi yake. Vipengele muhimu vya kuhakiki
katika fani ya ushairi ni kama vifuatavyo:
Mtindo
Jambo
la kuonyesha hapa ni kwamba iwapo shairi ni la kimapokeo ama ni la kisasa.
la kuonyesha hapa ni kwamba iwapo shairi ni la kimapokeo ama ni la kisasa.
Muundo.
Katika kuhakiki muundo wa shairi mhakiki inatakiwa aweke wazi mambo yafutayo:
Katika kuhakiki muundo wa shairi mhakiki inatakiwa aweke wazi mambo yafutayo:
1.
Idadi ya beti
Idadi ya beti
2.
Idadi ya mistari na aina ya vibwagizo
Idadi ya mistari na aina ya vibwagizo
3.
Idadi ya vipande
Idadi ya vipande
4.
Idadi ya mizani
Idadi ya mizani
5.
Aina na mpangilio wa vina
Aina na mpangilio wa vina
Wahusika
Ikiwa
shairi limehusisha wahusika ni vema pia mhakiki awabainishe
shairi limehusisha wahusika ni vema pia mhakiki awabainishe
Matumizi ya Lugha
Katika
kipengele hiki mhakiki huchunguza:
kipengele hiki mhakiki huchunguza:
1.
Mpangilio wa maneno. Mf. Wengi wari badala ya wari wengi
Mpangilio wa maneno. Mf. Wengi wari badala ya wari wengi
2.
Matumizi ya: Mazida – kurefusha neno
mfano, kiwembe badala ya wembe; Ikisari – kufupisha neno mfano siombe badala ya usiombe; Tabdila – kubadilisha mwendelezo wa neno mfano
kujitanuwa badala ya kujitanua.
Matumizi ya: Mazida – kurefusha neno
mfano, kiwembe badala ya wembe; Ikisari – kufupisha neno mfano siombe badala ya usiombe; Tabdila – kubadilisha mwendelezo wa neno mfano
kujitanuwa badala ya kujitanua.
3.
Matumizi ya methali, misemo na nahau
Matumizi ya methali, misemo na nahau
4.
Matumizi ya lugha ya picha
Matumizi ya lugha ya picha
5.
Matumizi ya tamathali za semi kama vile takriri, sitiari n.k
Matumizi ya tamathali za semi kama vile takriri, sitiari n.k
6.
Mbinu nyingine za kisanaa
Mbinu nyingine za kisanaa
Mhakiki
anapochunguza vipengele vya fani, jambo muhimu la kuzingatia ni jinsi vipengele
hivyo vinavyosaidia kuwasilisha maudhui.
anapochunguza vipengele vya fani, jambo muhimu la kuzingatia ni jinsi vipengele
hivyo vinavyosaidia kuwasilisha maudhui.
![]() |
Ushairi |
VIPENGELE VYA MAUDHUI
Ili
kuhakiki na kupata maudhui ya shairi inatakiwa kulisoma shairi kwa kulielewa
zaidi. Baada ya kupata picha fulani kuhusu shairi na kutafakari maana za maneno
muhimu, itatubidi tuelewe vipengele vya maudhui, ambavyo ni dhamira, mtazamo,
msimamo, falsafa ya mwandishi, ujumbe na maadili, migogoro na muktadha.
kuhakiki na kupata maudhui ya shairi inatakiwa kulisoma shairi kwa kulielewa
zaidi. Baada ya kupata picha fulani kuhusu shairi na kutafakari maana za maneno
muhimu, itatubidi tuelewe vipengele vya maudhui, ambavyo ni dhamira, mtazamo,
msimamo, falsafa ya mwandishi, ujumbe na maadili, migogoro na muktadha.
UHAKIKI WA MAIGIZO
Igizo
huhakikiwa kwa namna lilivyo katika maumbo yake yote mawili yaani fani na
maudhui.
huhakikiwa kwa namna lilivyo katika maumbo yake yote mawili yaani fani na
maudhui.
Vipengele vya Fani na
Maudhui katika Kuhakiki Maigizo
Maudhui katika Kuhakiki Maigizo
Fani
Uhakiki
wa fani katika maigizo unajihusisha na ufundi uliotumiwa. Ufundi huu
unajumuisha mambo kadhaa kama ifuatavyo:
wa fani katika maigizo unajihusisha na ufundi uliotumiwa. Ufundi huu
unajumuisha mambo kadhaa kama ifuatavyo:
Mtindo
Mtindo
ni sura ya maigizo inayojitokeza kupitia mpangilio wa maneno na vitendo.
Inabidi mhakiki achunguze kama kazi ni:
ni sura ya maigizo inayojitokeza kupitia mpangilio wa maneno na vitendo.
Inabidi mhakiki achunguze kama kazi ni:
1.
Mchezo wa jukwaani – wenye mpangilio wa mazungumzo baina ya watu na matendo
yao.
Mchezo wa jukwaani – wenye mpangilio wa mazungumzo baina ya watu na matendo
yao.
2.
Majigambo
Majigambo
3.
Vichekesho – mpangilio wa maneno yanayowasilisha ujumbe kwa kuchekesha.
Vichekesho – mpangilio wa maneno yanayowasilisha ujumbe kwa kuchekesha.
4.
Mazungumzo – maongezi ya kujibizana baina ya watu.
Mazungumzo – maongezi ya kujibizana baina ya watu.
5.
Ngonjera – mpangilio wa tungo za kishairi ambapo watu wawili au makundi mawili
hukinzana.
Ngonjera – mpangilio wa tungo za kishairi ambapo watu wawili au makundi mawili
hukinzana.
Miviga – sherehe za kitamaduni kama vile matambiko
Pamoja
na haya, mtindo hutegemea lengo la maigizo ambalo laweza kuwa kuelimisha,
kukejeli, kuburudisha, kuonya, kukosoa na kadhalika.
na haya, mtindo hutegemea lengo la maigizo ambalo laweza kuwa kuelimisha,
kukejeli, kuburudisha, kuonya, kukosoa na kadhalika.
Mandhari
Mazingira
ya kutendea ni kipengele muhimu cha fani. Mhakiki hana budi kujiuliza iwapo
utendaji unadhihirisha wakati au mahali halisi. Jambo hili huweza kutekelezwa
kupitia vifaa, maleba, maneno n.k.
ya kutendea ni kipengele muhimu cha fani. Mhakiki hana budi kujiuliza iwapo
utendaji unadhihirisha wakati au mahali halisi. Jambo hili huweza kutekelezwa
kupitia vifaa, maleba, maneno n.k.
Wahusika
Maswali
ya mhakiki kuuliza ni:
ya mhakiki kuuliza ni:
1.
Wamejitokeza kikamilifu?
Wamejitokeza kikamilifu?
2.
Wanaaminika?
Wanaaminika?
Matumizi ya lugha
Vigezo
anavyotumia mhakiki kuchunguza lugha ni:
anavyotumia mhakiki kuchunguza lugha ni:
1.
Kama usemaji ni wa kisanaa, yaani unatumia picha, tamathali za semi, methali,
nahau n.k.
Kama usemaji ni wa kisanaa, yaani unatumia picha, tamathali za semi, methali,
nahau n.k.
2.
Kama lugha imetumika vile inavyotumiwa katika jamii. Mfano: kiimbo, mkazo,
miguno, vihisishi n.k.
Kama lugha imetumika vile inavyotumiwa katika jamii. Mfano: kiimbo, mkazo,
miguno, vihisishi n.k.
3.
Matumizi ya maneno ya ajabu kama yale yanayotumiwa na waganga.
Matumizi ya maneno ya ajabu kama yale yanayotumiwa na waganga.
Maleba na vifaa
Hivi
huakisi mandhari na husaidia kuzua mukatadha. Kwa hiyo ni muhimu kuchunguza
kama vimetumiwa ipasavyo.
huakisi mandhari na husaidia kuzua mukatadha. Kwa hiyo ni muhimu kuchunguza
kama vimetumiwa ipasavyo.
Matumizi ya ala
Matumizi
ya ala kama ngoma, baragumu, au sauti zingine ili kuamsha hisia za hadhira ni
jambo muhimu kuchunguza.
ya ala kama ngoma, baragumu, au sauti zingine ili kuamsha hisia za hadhira ni
jambo muhimu kuchunguza.
Mbinu nyingine
Mhakiki
anapaswa pia kuchunguza matumizi ya nyimbo, uchezaji ngoma, usimulizi na mbinu
nyingine katika kuibua hisia za watazamaji.
anapaswa pia kuchunguza matumizi ya nyimbo, uchezaji ngoma, usimulizi na mbinu
nyingine katika kuibua hisia za watazamaji.
Maudhui
Kwa
upande wa maudhui, mhakiki wa maudhui hutakiwa kuchunguza vipengele vyote vya
kimaudhui ambavyo ni dhamira, migogoro, maadili, mtazamo na msimamo wa fanani
pamoja na ujumbe bila kusahau kipengele cha falsafa. Yote hayo kwa pamoja ndiyo
humsaidia mhakiki kubaini ukinzani wa igizo na maisha halisi ya jamii ambayo huwa
ndiyo hadhira ya igizo hilo.
upande wa maudhui, mhakiki wa maudhui hutakiwa kuchunguza vipengele vyote vya
kimaudhui ambavyo ni dhamira, migogoro, maadili, mtazamo na msimamo wa fanani
pamoja na ujumbe bila kusahau kipengele cha falsafa. Yote hayo kwa pamoja ndiyo
humsaidia mhakiki kubaini ukinzani wa igizo na maisha halisi ya jamii ambayo huwa
ndiyo hadhira ya igizo hilo.
3 Comments
i like science subject
Nimependa summary ya uhakiki wa ushairi na migizo
Mbona hakuna uhakiki wa ngonjera